Posts

FORM FIVE SELECTION 2016 CHECK HERE

Image
TAARIFA KWA UMMA 24-JUNI-2016. OR-TAMISEMI inawatangazia majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi kwa mwaka 2016. Wanafunzi waliochaguliwa ni kutoka shule za Serikali na zisizo za Serikali. Jumla ya wanafunzi 65,720 wakiwemo wasichana 29,457 na wavulana 36,263 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi. Kati ya wanafunzi waliochaguliwa 34,064 wakiwemo wasichana 13,466 na wavulana 20,598 sawa na asilimia 52 watajiunga na masomo ya Sayansi na Hisabati; na wanafunzi 30,897 wakiwemo wasichana 15,445 na wavulana 15,452 sawa na asilimia 47 wamechaguliwa kusoma masomo ya Sanaa na Biashara na wanafunzi 759 wakiwemo wasichana 220 na wavulana 539 sawa na asilimia 1 wamechaguliwa kujiunga na vyuo vya Ufundi. Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano mwaka 2016 wataanza muhula wa kwanza tarehe 11 Julai, 2016 na hakutakuwa na mabadiliko yoyote ya shule. Wanafunzi wote wanatakiwa kuripoti katika sh

TANZANIA has started to build its own helicopters in a project that will see the first batch of such choppers taking into the sky sometimes in 2018.

Image
Already, the prototype model, a two-seater aircraft is in its final stages of completion at the Mechanical and Engineering Department of the Arusha Technical College, which runs a fully-fledged factory producing various forms of machinery, including a prototype motor vehicle and a number of industrial engines.But it is the Tanzanian-made new helicopter that seems to be turning heads here; “We are complementing President Magufuli’s industrialisation policy in pioneering the first locally made helicopters that will be available to ordinary residents at affordable prices,” explained the man behind the ATC chopper project, Engineer Abdi Mjema.The Permanent Secretary in the Ministry of Education, Science and Technology, Ms Maimuna Tarishi, who also toured the project over the weekend seemed surprised at the development and wanted to know when exactly the chopper will hit the skies.“We are contacting the Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA) for the permission to fly the chopper for trial

List ya nchi 11 zinazoongoza kwa amani na usalama duniani

Image
List ya nchi zenye usalama zaidi duniani kwa mwaka 2016 imetoka hivi karibuni ambapo nchi 11 zimetajwa kuongoza kwa kuwa na usalama na amani zaidi. List hiyo ilihusisha mataifa 163 ambapo ilijulikana yale yanayoongoza kwa amani na usalama pamoja na yale ambayo ni hatari zaidi kuishi kutokana na hali ya usalama. Toleo la 10 la kila mwaka lililotolewa June 8 2016 limetaja viwango vya amani na usalama kupitia system ya ramani  shirikishi ya mtindo wa rangi za kujificha, kila nchi ilitolewa alama kati ya 5, nchi zenye alama chini ya 5 ndio zenye hali kubwa ya usalama na amani na zilizoizidi namba 5 ndizo hatari zaidi. Ulifanyika uchambuzi wa mambo 23 chini ya makundi matatu, Usalama na amani ya taifa, Migogogro ya ndani na nje ya nchi pamoja na huduma za kijeshi. Nchi ya Iceland inatajwa kuongoza kwa kuwa na amani zaidi kutokana na utulivu wa jamii yake. Nchi za ulaya zinaongoza kutokana na kutokuwa na migogoro ya ndani na nje pamoja ya hali ya utulivu kwa ujumla, japokuwa Afrika inasif

Uliiona picha ya Diamond Platnumz kutoboa pua?! ukweli ninao hapa

Image
Kwa saa kadhaa zimeenea taarifa za mwimbaji staa wa bongofleva Diamond Platnumz kuonekana katoboa pua, hii habari imepewa nguvu kutokana na picha aliyoipost Diamond mwenyewe kwenye Instagram akionekana katoboa pua. Ukweli ukoje? …ukweli ni kwamba Diamond hajatoboa pua kama wengi walivyodhani ambapo Meneja wake aitwae Sallam aliwajibu hivi mashabiki walioanza kuuliza >>> ‘Usiamini kila unachoona kwenye picha au unachoambiwa, mlikuwa mmelala sana amewaamsha kidogo’ Maneno ya Meneja Sallam yanamaanisha kwamba sio kweli Diamond katoboa pua, ni mchezo tu na baada ya hiyo picha ya kutoboa pua Diamond aliweka picha nyingine inayoonekana hapa chini akiwa fresh kabisa watu wasiendelee kupanic. ULIIKOSA SHOW YA DIAMOND ILIYOVUNJA REKODI YA MR NICE MAREKANI? ITAZAME HAPA CHINI

Wizara ya Elimu Sayansi,Teknolojia na Ufundi inakanusha taarifa iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari 'NDALICHAKO NA WALIMU TZ'.

Image
Wizara ya Elimu Sayansi,Teknolojia na Ufundi inakanusha taarifa iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari 'NDALICHAKO NA WALIMU TZ'. Taarifa hiyo inadai kwamba Waziri wa Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi Prof. Joyce Ndalichako amesema kuwa walimu wanaandaliwa sare watakazovaa wakati wa kazi. Tunapenda kuwafahamisha umma kuwa taarifa hizi si za kweli. Aidha wizara inawataka watu wote wanaoeneza taarifa za kizushi aina hii waache kufanya hivyo ili kuepusha usumbufu unaojitokeza. Aidha Hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa watakaobainika kuanzisha na kueneza ushushi huu.

Magazeti ya Tanzania yalichoandika leo April 8 2016 kwenye, Udaku, hardnews na michezo:

Magazeti ya Tanzania yalichoandika leo April 8 2016 kwenye, Udaku, hardnews na michezo: KUYAANGALIA BOFYA HAPA

Sasa hivi sio wewe kuwafata TANESCO wakuunganishie Umeme, ni wao ndio wanatakiwa kukufata

Image
Awamu ya tano ya Rais Magufuli imeambatana na maamuzi mapya au yaliyoongezewa ubunifu na nguvu kubwa ya ufatiliaji ambapo kwenye wizara ya nishati boss Profesa Muhongo cheo chake kikiwa ni Waziri wa nishati na madini amekuja na hii mpya. Tulizoea kuona Taasisi za kibishara kama Benki na taasisi nyingine ndio zinafata Watu kuomba wanunue bidhaa zao au kujiunga na benki ila sasa hivi imehamishiwa TANESCO maana siku zote ilikua Wananchi ndio wananyenyekea TANESCO wawaunganishie umeme kwenye nyumba zao, Waziri Muhongo ameagiza na kuanzia sasa TANESCO ndio watakua wanafata watu kuomba kuwaunganishia umeme. Profesa Muhongo amekuja na hii mpya na ninamnukuu >>> ‘TANESCO wanaagizwa kuanzia sasa wawafate Wananchi hukohuko vijijini wakiwa na Wakusanya fedha na stakabadhi zao Wananchi walipie hukohuko vijijini, labda ndugu zangu hamkua mnajua… kazi moja tunaifanya TANESCO sasa hivi, ukitaka kuendelea na umeneja tunakutathmini kila baada ya miezi mitatu‘ ‘Tathmini yetu ina vigezo vitat