Posts

Showing posts from March 13, 2016

CHOMBEZO FUPI INAITWA ««JAMANI ANKO»» ISOME HAPA

CHOMBEZO FUPI: JAMANI ANKO MTUNZI: George Iron Mosenya SIMU:0655727325 Nilitamani muda wa vipindi darasani umalizike ili iweze kutimiza ahadi niliyokuwa naisubiri kwa siku nyingi. Mwalimu alikuwa akifundisha lakini ni kama nilikuwa sielewi wala sisikii alichokuwa anaelezea. Mawazo yangu yote yalikuwa kwa Madam Jesca. Siku hiyo nilijisemea kuwa iwe isiwe lazima nimweleze ukweli na ikibidi siku hiyo hiyo yatimie ninayoyawaza kila kukicha. Madam Jesca alikuwa ni mwalimu aliyekuwa akitufundisha kwa muda tu baada ya kuwa amemaliza kidato cha sita. Wakati huo sisi tulikuwa kidato cha nne. Somo alilokuwa akitufundisha ni Kiswahili. Hatimaye mwalimu akatoka na baada ya nusu saa nikaondoka kuelekea nyumbani kwa madam Jesca. Niliingia baada ya kuwa nimegonga hodi. “We Joshua mbona muda wa vipindi hivi we umekuja huku..” aliniuliza huku macho yake yakionyesha mshangao wa waziwazi. Kanga yake aliyovaa ilikuwa imelowana na hivyo kusababisha niuone mstari wa chupi. Na kama hiyo haitoshi

SOMA HII.....ITAKUTIA MOYO KATIKA MAISHA YAKO

Image
Watu wengi wameshindwa kufanikiwa katika maisha sababu ya vikwazo walivyokutana navyo na kusababisha kushindwa kufanya jambo fulani,hivyo wamejikuta wakianguka na kukata tamaa ,hivyo basi naomba nikutie moyo Leo, 1.Kushindwa kwako jana haimaanishi utashindwa na Leo,inuka jipanguse na songa mbele. 2.Usiiishi Jana yako ila itumie kama njia ya kujifunza ili leo usikosee palepale ulipokosea Jana. 3.Kilichofanyika,kishafanyika hauna Uwezo wa kubadilisha jambo lililofanyika ila una Uwezo wa kubadilisha jambo unalolifanya Leo ili uwe na kesho nzuri. 4.Tambua hauwezi kuwa na kesho nzuri kama unatumia muda wako mwingi kuifikiria Jana yako.Tumia mda wako mwingi kuifikiri Leo maana ndiyo uliyonayo. 5.Kataa msamiati nashindwa au siwezi katika maisha yako,pamoja na vikwazo  vyote bado tambua inawezekana. 6.Kushindwa sio maisha yako ila ni sehemu ndogo tu ya maisha yako,hivyo tambua hapo ulipo unapita tu kuna mazuri yanakuja mbele. 7.Hata usiku wa manane huisha na jua likachomoza,hivyo hata m